vaccine image

Chanjo yenye virusi hai vya mdondo vya I-2 inayohimili joto vinavyo kinga kuku dhidi ya ugonjwa wa mdondo. Mdondo ni ugonjwa wa kuambukiza kwenye kuku na jamii zingine za ndege unaosababishwa na virus aina ya para-myxovirus. Ndege wanopata ugonjwa huu ni kuku, batamzinga, bukini, bata, kanga, kware and ndege wengine wasiofugwa na waliohifadhiwa. Dalili zake ni pamoja na kuharisha kinyesi cha kijani, mafua makali, kizunguzungu na hatimaye kifo. TEMEVAC inazalishwa kulingana na viwango vya ubora chini ya muongoza wa viwango vya ubora wa ISO 9001:2015 pamoja na viwango na miongozo ya Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH).