Kituo cha magonjwa yanayoambukiza na bayoteknolojia

OFISI ZA MAKAO MAKUU

WAKALA YA MAABARA YA VETERINARI TANZANIA

Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) ni Wakala ya Serikali chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.  Ofisi za Makao makuu ya Wakala yapo eneo la Temeke-Dar es Salaam pembezoni mwa barabara ya Mandela. Makao Makuu ya Wakala yana ofisi za Mtendaji Mkuu, Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Mameneja na watumishi wote wa Makao Makuu.

Anwani

Mtendaji Mkuu,

S.L. P 9254,

Majengo ya Veterinari, 131 Barabara ya Nelson Mandela,

Temeke- Dar es Salaam,Tanzania

Simu: +255 22 2861152
Nukushi: +255 22 2864396
Baruapepe: info@tvla.go.tz

KITUO CHA MAGONJWA AMBUKIZI NA BiOTEKNOLOJIA (CIDB)

Kituo cha Magonjwa Ambukizi na Bioteknolojia ni mojawapo ya vituo vya Wakala ambacho kipo katika eneo la Temeke-Dar es Salaam, pembezoni mwa barabara ya Nelson Mandela. Hii ni maabara ya rufaa ya wanyama nchini katika uchunguzi na utambuzi wa magonjwa ya wanyama yanayosababishwa na virusi. Maabara hii pia ni kituo cha Biotechnolojia ikifanya tafiti mbalimbali za chanjo na utambuzi wa magonjwa. Kituo hiki kina ithibati ya kimataifa (ISO/IEC 17025:2017) ya utambuzi wa magonjwa ya wanyama.

 

Kwa mawasiliano;

 

Meneja,

Kituo cha Magonjwa ambukizi na Bioteknolojia,

S.L. P 9254,

Majengo ya Veterinari, 131 Barabara ya Nelson Mandela,

Temeke-Dar es Salaam,Tanzania

Simu: +255 22 2861152
Nukushi: +255 22 2864396
Baruapepe: cidb@tvla.go.tz